Kiongozi mkuu wa China Xi Jinping leo amesema, hivi leo China imesimama kidete kwenye mashariki ya dunia, hakuna nguvu yoyote inayoweza kutikisa hadhi ya China, na hakuna nguvu yoyote inayoweza kuzuia hatua ya kusonga mbele ya wananchi wa China na Taifa la China.
Rais Xi Jinping amedhihirisha kuwa kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China kumebadilisha kabisa hatma mbaya ya umaskini na udhaifu ya China tokea zama za karibu, na Taifa la China limefuata njia pana ya kutimiza ustawishaji mkubwa.
Katika miaka 70 iliyopita, watu wa makabila mbalimbali wa China wameungana kwa nia moja na moyo mmoja katika kufanya juhudi kubwa za kushinda taabu, na wamepata mafanikio makubwa ya kuwashangaza watu wa dunia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |