• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tamasha kubwa la kusherehekea Miaka 70 ya Jamhuri ya Watu wa China limefanyika Beijing

    (GMT+08:00) 2019-10-01 21:45:22

    Tamasha kubwa la kusherehekea Miaka 70 ya Jamhuri ya Watu wa China limefanyika Beijing

    Rais Xi Jinping na viongozi wengine wa Chama na serikali wamefika kwenye jukwaa la viongozi lililoko kwenye roshani ya Tian An Men, wakisherehekea pamoja na wananchi usiku wa sikukuu ya taifa.

    Saa mbili usiku juu ya alama, Jumba la Simu ya Upepo la Beijing lilipiga muziki mwororo wa "Mashariki Kwekundu", ambapo mjumbe wa Ofisi ya Siasa ya Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China ambaye pia ni Katibu wa Kamati ya Chama ya Beijing Bw. Liu Qi alitangaza kwamba, Tamasha la kusherehekea sikukuu ya taifa linaanza.

    Tamasha hilo limegawanywa katika sehemu nne: "Wasifu wa Bendera ya Taifa", "Tunasonga Mbele kwenye Njia Pana", "Kwenye Ardhi kubwa Yenye Matumaini", na "Kushika Usukani wa Zama Mpya", ambapo watu wanaimba huku wakicheza ngoma kwa furaha, na fashifashi za kupendeza zikirushwa angani.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako