Timu ya taifa ya Tanzania ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 maarufu kwa jina la Ngorongoro Heroes, leo Oktoba 2 2019 watacheza mchezo wao wa nusu fainali ya michuano ya CECAFA dhidi ya Sudan. Mchezo huo watacheza baada ya kutinga hatua hiyo kwa kuiondoa Uganda ambao ndio wenyeji kwa kuwafunga magoli 4-2, wachezaji wa Ngorongoro Heroes Kelvin John na Andrew Simchimba ndio wachezaji hatari kwa kufumania nyavu wote wakifunga hart-trick.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |