• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rwanda: Biashara ya ulimwengu inatarajiwa kukua kwa kasi ya chini

    (GMT+08:00) 2019-10-02 19:43:41
    Biashara ya ulimwengu inatarajiwa kukua kwa kasi ya chini mwaka huu na mwaka ujao kuliko ilivyotarajiwa hapo awali.

    Hii inalaumiwa kwa kuongezeka kwa mvutano wa kibiashara na kutokuwa na Brexit, kulingana na Shirika la Biashara Ulimwenguni (WTO).

    Biashara ya ulimwengu katika uuzaji inatarajiwa kuongezeka kwa asilimia 1.2 tu mwaka huu, chini ya kiwango cha ukuaji wa asilimia 2.6 iliyotarajiwa Aprili, WTO imesema katika taarifa iliyotolewa.

    Biashara ya ulimwengu inatabiriwa kufika asilimia 2.7 mwaka ujao, chini ya asilimia 3 iliyotabiriwa hapo awali.

    Mkurugenzi Mkuu wa WTO Roberto Azevêdo amesema mtazamo mbaya wa biashara ndio unavuja moyo.

    WTO ambayo inashughuka na sheria za biashara za kimataifa, ilitahadharisha kwamba kushuka kwa kiwango cha chini kunaweza kupunguza nafasi mpya za ajira na kuifanya kuwa ngumu kwa makampuni kutoa bidhaa na huduma kwa masoko kwa ajili ya mauzo ya nje.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako