Waziri mkuu wa Uingereza Boris Johnson ametangaza kuwa Uingereza itajitoa Umoja wa Ulaya tarehe 31 Oktoba bila ya makubaliano yoyote, ikiwa mapendekezo yake ya mwisho yaliyowasilishwa kwenye Umoja wa Ulaya yatakataliwa. Bw. Johnson amesisitiza kuwa mapendekezo yaliyowasilishwa kwenye Umoja wa Ulaya hayatamaanisha kutakuwa na ukaguzi wowote kwenye au karibu na mpaka kati ya Ireland ya Kaskazini na jirani yake Jamhuri ya Ireland.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |