Vyama hivyo vinavyoendelea kubadilisha maisha ya watu na kufanikisha ndoto za wananchi na hasa wenye kipato cha chini ndani ya jamii ya watanzania,vinalenga kuwainua kiuchumi kwa kuwahakikishia kipato endelevu kitakachowawezesha kumudu gharama za maisha.
Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika wa Akiba na Mikopo Tanzania,Dk Gervas Machimu,jana alisema vya ma hivyo vitakutana katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa Ushirika wa Akiba na Mikopo (Saccos) ambayo mwaka huu yanafanyika katika hoteli ya Springs Corridor jijini Arusha.
Kulingana na Dk Machimu,kupitia siku hiyo,vyama vyote vya ushirika na mikopo Tanzania,vinatafakari namna iliyo bora ya kufikisha huduma za fedha vijijini na kutatua changamoto za mitaji kwa wananchi.
Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Ushirika wa Akiba na Mikopo hufanyika kila alhamisi ya tatu ya mwezi Oktoba.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |