Huduma za China UnionPay ambayo ni Kampuni kubwa zaidi ya ulipaji kwa kutumia kadi za benki nchini China, zimeenea katika nchi na sehemu 176 duniani. Taarifa iliyotolewa na kampuni hiyo imesema, watoa huduma katika nchi za Bosnia, Herzegovina na Chile wameanza kukubali kadi za UnionPay kwa mara ya kwanza. Kadi zinazotolewa na Kampuni hiyo ambayo makao makuu yako mjini Shanghai, sasa zinakubaliwa na watoa huduma zaidi ya milioni 28 duniani, na imetoa kadi milioni 120 katika nchi na sehemu 57 duniani, zikiwemo Bahrain na Madagascar.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |