Tume ya haki za binadamu ya Iraq IHCHR imesema watu 19 wameuawa, na wengine zaidi ya 1,000 wamejeruhiwa katika siku ya tatu ya maandamano yenye vurugu yaliyotokea huko Baghdad, pamoja na miji mingine ya katikati na mikoa ya kusini nchini humo. Mjumbe wa tume hiyo Bw. Al-Halfi amesema vikosi vya usalama vimewakamata waandamanaji 210, lakini vimewaachia huru 154 kati yao, wakati wengine bado wako kwenye vituo wakishikiliwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |