Chama cha kijamaa PS kinachoongozwa na waziri mkuu wa Ureno Antonio Costa kinatarajiwa kushinda kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika jana kwa kupata asilimia 36.7 ya kura. Baada ya asilimia 97.1 ya kura zote kuhesabiwa, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi hiyo imesema chama kikuu cha upinzani PSD kiko katika nafasi ya pili kwa kupata asilimia 28.6.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |