Idadi ya watu waliouawa kwenye maandamano yaliyotokea Baghdad na miji mingine ya Iraq imeongezeka na kufikia 104, huku watu zaidi ya elfu 6 wakijeruhiwa wakiwemo walinzi usalama wengi. Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari, msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani Bw. Saad Maan amesema watu wasiojulikana wenye silaha jana walishambulia ofisi za vyombo vya habari vya ndani na nje, na uchunguzi kuhusu mashambulizi hayo unaendelea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |