Rais Barham Salih wa Iraq amewataka waandamanaji nchini humo kushiriki kwenye mazungumzo ya kitaifa ili watu wafahamishwe kuhusu hatua za mageuzi. Rais Salih pia amehimiza kuzuia maandamano kuzidi kuwa makubwa ili kuepusha watu kutoka nje kuingilia mazungumzo ya kitaifa. Pia amesema vitendo vya kuwashambulia watu wanaoandamana kwa amani na askari wa usalama, na vya kuvilenga vyombo vya habari na wafanyakazi wake, havikubaliki nchini Iraq. Amesema Iraq inatakiwa kuwa nchi ya kidemokrasia, ambapo haki na uhuru vinaheshimwa na katiba inafuatwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |