Chansela wa Ujerumani Bibi Angela Merkel amezungumza na rais Volodymyz Zelensky wa Ukraine kwa njia ya simu, na kujadiliana kuhusu uwekezano wa kufanyika mkutano wa kilele wa kushughulikia suala la Ukraine. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na serikali ya Ujerumani, viongozi hawa wamekubaliana kuwa mazingira ya kufanyika kwa mkutano kama huo yapo, baada ya Kundi la Mawasiliano la Pande Tatu kufikia makubaliano kuhusu kumaliza mgogoro katika mashariki mwa Ukraine.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |