Bondia Patrick Day wa Marekani anapigania maisha yake baada ya maumivu aliyopata kichwani kwenye mchezo wa jana, aliopoteza kwa knockout. Jana mwanamasumbwi huyo alifanyiwa upasuaji wa ubongo mjini Chicago, na sasa hali yake iko mahututi. Bondia aliyemtwanga knockout Charles Conwell, amejitokeza kwenye mitandao ya kijamii na kuwataka mashabiki wake wamwombee Patrick apone.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |