• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania: Saccos chaazimia kujenga kitega uchumi cha kisasa

    (GMT+08:00) 2019-10-15 16:54:33
    Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Hazina (Saccos) kimeazimia kujenga kitega uchumi cha kisasa kwa gharama ya Sh52 bilioni kupitia mradi wa Njedengwa uliopo Jijini Dodoma.

    Mradi huo unalenga kukuza uchumi wa Mkoa wa Dodoma na Taifa kupitia kodi.

    Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Bodi wa chama hicho, Aliko Mwaiteleke wakati wa Mkutano Mkuu wa mwaka uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Hazina.

    Amesema mradi huo upo katika hatua za mwisho za utekelezaji wake.

    Mwaiteleke amesema mpaka sasa upembuzi yakinifu wa mradi huo utakaojengwa kwa njia ya ubia kati ya Hazina Saccos na mwekezaji kwenye eneo lenye ukubwa wa ekari 22 kupitia utaratibu wa Jenga, Endesha na Hamisha (Build, Operate and Transfer - BOT), mwekezaji atagharamia ujenzi wote na kuendesha kwa muda ambao utakubaliwa ndani ya mkataba.

    Amesema mradi huo unasimamiwa na Kamati ya watu saba wakiongozwa na Profesa Esta Eshengoma kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na wajumbe wake kutoka Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru), Bodi ya Manunuzi ya Umma (PSPTB), Kituo Cha Uwekezaji (TIC) na Chuo Kikuu cha Ardhi ambao kwa sasa wanafanya kazi ya kusaka mwekezaji ili kufanikisha mradi huo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako