• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kikundi kipya cha timu ya madaktari ya China kuanza kutoa huduma za afya nchini Rwanda

    (GMT+08:00) 2019-10-16 08:52:41

    Hafla ya kupokezana zamu kati ya kikundi cha 19 na cha 20 cha madaktari wa China imefanyika katika ubalozi wa China huko Kigali, mji mkuu wa Rwanda.

    Kikundi cha 19 cha madaktari wa China kilichotoa huduma za afya katika hospitali ya Masaka ya Kigali na hospitali ya Kibungo iliyoko kusini mashariki kimefanikiwa kumaliza majukumu ya mwaka mmoja nchini Rwanda baada ya kufanya upasuaji zaidi ya 500.

    Kikundi hicho pia kimechangia vifaa vya matibabu na vitu mbalimbali vya afya kwa hospitali za huko, huku kikitoa huduma za bure za afya kwa wanavijiji na kutoa mchango katika kuboresha huduma za afya na usimamizi nchini humo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako