Shughuli kuu ya uzinduzi ilifanyika katika kituo cha SGR cha katika eneo la Mai Mahiu.
Aidha huduma ya treni ya kubeba abiria itaanza rasmi kesho alhamisi huku ile ya uchukuzi wa mizigo ikianza baada ya miezi kadhaa ijayo.
Huduma hiyo ya uchukuzi wa abiria itapatikana tu katika vituo vinne kati ya 12 katika awamu hiyo ya SGR.
Vituo hivyo ni pamoja na Ongata Rongai, Ngong, Mai Mahiu na Suswa.
Katika kipindi cha miezi miwili iliyopita, kampuni ya China Communication and Construction Company iliyojenga reli hiyo imekuwa ikiendesha safari za majaribio kama sehemu ya maandalizi kwa uzinduzi wa leo Jumatano.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |