Waziri wa mambo ya nje wa nchi hiyo Bw. Mohammad Javad Zarif amesema Ulaya imeshindwa kutekeleza ahadi kuhusu nyuklia katika kulinda maslahi ya Iran. Bw. Zarif amesema kufuatia kujitoa kwa Marekani kwenye makubaliano ya nyuklia ya mwaka 2015 JCPOA, Iran iliendelea kufuata makubaliano hayo, lakini Ulaya ilishindwa kuheshimu ahadi zake. Amesema kama ikiwa pande zinazohusika hazichukui hatua za kulinda maslahi ya Iran, Iran itachukua hatua zaidi kupunguza ahadi zake.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |