Rais Donald Trump wa Marekani amesema kutokana na "uhasama" wa Chama cha Democrats na vyombo vya habari, atachagua sehemu nyingine badala ya klabu yake binafsi ya golf katika jimbo la Florida kwa ajili ya mkutano wa kundi la nchi saba G7 wa mwaka kesho. Ikulu ya Marekani tarehe 17 ilitangaza kuwa mkutano huo utafanyika katika Klabu ya Golf ya Doral ya Trump iliyoko mjini Miami, Florida. Uamuzi huo ulikosolewa na Chama cha Democrats, vyombo vya habari na hata baadhi ya wanachama wa Chama cha Republican.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |