Bao pekee lililofungwa na Mnamibia Sadney Urikhob liliiwezesha Yanga kuibuka na ushindi katika mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Mbao FC iliyochezwa jana kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza. Kwa matokeo hayo, Yanga ambayo imecheza mechi nne, imefikisha pointi 7 sawa na Mbao FC, lakini imepanda hadi nafasi ya 10 kwenye msimamo wa Ligi hiyo huku wenyeji wao wakibakia katika nafasi ya 13.