• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Telkom nchini na Airtel kuungana mwaka ujao

    (GMT+08:00) 2019-10-23 19:51:40
    Kampuni ya mawasiliano ya Telkom nchini Kenya imesema inatarajia kuungana na ile ya Airtel mwaka ujao.

    Mkurungezi mkuu wa Telkom Mugo Kibati ameiambia kamati ya seneti ya mawasailiano na Teknolojia kuwa wanasubiri mamlaka husika kutoa idhini ili kuanza mchakato w muuungano.

    Muungano wa kampuni hizo mbili za mawasiliano unatarajiwa kutoa ushindani kwa kampuni ya Safaricom ilio na mgao mkubwa wa soko nchini Kenya.

    Serikali inamiliki asilimia 40 ya hisa za Telkom nayo kampuni ya Helios inamiliki asilimia 60.

    Hata hivyo mamlaka ya mawasiliano nchini Kenya imesema kuwa lazima kampuni hizo zilipe madeni yao yote kabla ya kuungana.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako