Rais Abdel-Fattah al-Sisi wa Misiri na waziri mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed wamekubaliana kurejesha mara moja kazi ya kamati ya kiufundi ya bwawa la GERD.
Taarifa iliyotolewa na msemaji wa ikulu ya Misri Bassam Rady inasema, kamati hiyo inalenga kufikia makubaliano ya mwisho ya kanuni ya kujaza na kuendesha bwawa hilo.
Makubaliano hayo yamefikiwa katika mkutano kati ya viongozi hao wawili kando ya mkutano wa kilele kati ya Russia na Afrika unaofanyika Sochi, nchini Russia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |