Mkutano wa 18 wa siku mbili wa Harakati ya Nchi Zisizofungamana na Upande Wowote umefungwa jana huko Baku, Azerbaijan. Mkutano huo ulipitisha Azimio la Baku inayoelekeza maendeleo ya baadaye ya Harakati hiyo, na kusisitiza kwamba itaongeza nguvu zaidi na ufanisi, kukuza utaratibu wa pande nyingi, amani na maendeleo ya kikanda.
Azimio hilo linasisitiza kwamba nchi wanachama zinaunga mkono mfumo wa kimataifa ambao Umoja wa Mataifa kama kiini chake na zinaheshimu ukamilifu wa nchi na usawa wa uhuru, uhuru wa kisiasa na kutoingilia katika mambo ya ndani ya kila mmoja, na nchi wanachama zitaongeza juhudi ili kupambana na ugaidi wa aina zote.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |