Mwanariadha Alphonce Simbu amefanikiwa kupeperusha vyema bendera ya Tanzania katika mashindano ya majeshi ya Dunia yaliyomalizika jana hapa nchini China, na kuitoa kimasomaso nchi hiyo kwa kujinyakulia medali ya Fedha. Mwanariadha huyo akiwakilisha Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, alimaliza baada kukimbia kwa saa 2:11:16 huku akiwaahinda wakimbiaji wengine 95 kutoka nchi zaidi ya 30. Katika mbio hizo mshindi wa kwanza aliyejizolea medali ya dhahabu ni Luche Sumi kutoja Bahrain aliyekimbia kwa saa 2:08:28, na mshindi wa tatu aliyeondoka na shaba ni mwanariadha kutoka Rwanda John Hakizimana akiyekimbia kwa karibu nyuma ya Simbu kwa saa 2:11:19.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |