Baada ya kutoa mpango wa kufanya uchaguzi mkuu mapema tarehe 12 mwezi Desemba, uungaji mkono wa waziri mkuu wa Uingereza Bw. Boris Johnson amekuwa na ongezeko kwenye kura za maoni zilizotangazwa Jumapili.
Gazeti la Sunday Times limesema, kutokana na matokeo yaliyotolewa na mashirika matano ya upigaji kura, chama cha wahafidhina kitaibuka na wingi zaidi kwenye uchaguzi mkuu.
Habari zimesema Jumatatu alasiri Bw. Johnson atalitaka bunge likubali kuitishwa kwa uchaguzi mkuu mapema, kwani anajua mpango wake utafanikiwa tu ikiwa unaungwa mkono na wapinzani wa kutosha.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |