Shirika la habari la Korea Kaskazini KCNA limeripoti kuwa, mkuu wa Kamati ya Amani ya Asia na Pasifiki Bw. Kim Yong Chol ameikosoa Marekani kwa kuendelea na sera za uhasama dhidi ya Korea Kaskazini. Amesema Marekani si kama tu haijabadilisha mienendo yake kwa kuitikia matakwa ya Korea Kaskazini, bali inajaribu kutumia "njia za kijanja na kiovu zaidi" kuitenga Korea Kaskazini na kukwamisha maendeleo yake. Ameihimiza Marekani kuandaa mpango mpya wa kufanya mazungumzo na Korea Kaskazini.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |