Rais Vladmir Putin wa Russia jana alizungumza kwa njia ya simu na chansela wa Ujerumani Bibi Angela Merkel, wakijadili hali ya Syria. Habari kutoka Ikulu ya Russia Kremlin zimesema viongozi wa nchi hizo wanaona kwa kauli moja kuwa, utekelezaji wa makubaliano yaliyofikiwa kati ya Russia na Uturuki unasaidia utulivu wa hali ya kaskazini mashariki mwa Syria, na kuhimiza mchakato wa siasa nchini humo ikiwa ni pamoja na kazi ya kamati ya katiba ya Syria itakayoanzishwa tarehe 30 mwezi huu huko Geneva.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |