Jeshi la Korea Kusini limesema Korea Kaskazini ilirusha vitu viwili visivyojulikana kwa upande wa eneo la bahari lililoko mashariki ya Peninsula hiyo. Kituo cha mnadhimu mkuu wa Jeshi la Korea Kusini kimesema, pande hizo mbili zinaendelea kufanya utafiti wa kina kuhusu hali halisi ya vitu hivyo, na kwamba jeshi la nchi hiyo linafuatilia kama Korea Kaskazini itarusha tena au la, na kuweka tahadhari juu ya mwelekeo wa tukio hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |