China imerusha satelaiti mpya ya uchunguzi wa dunia, Gaofen-7, ambayo itafanya kazi muhimu katika utafiti na uchoraji ramani, ujenzi wa miji na vijiji na uchunguzi wa kitakwimu. Mamlaka ya Anga za Juu ya China CNSA imesema satelaiti hiyo ilirushwa na roketi ya Long March-4B ambayo pia ilirusha satelaiti nyingine tatu za kibiashara na kisayansi ikiwemo moja kwa ajili ya Sudan.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |