Wataalamu zaidi ya elfu 11 kutoka zaidi ya nchi 150 duniani wametangaza kuwepo kwa hali ya tahadhari kuhusu hali ya hewa, na kuonya kuwa binadamu wanakabiliwa na janga kama watashindwa kutatua msukosuko wa hali ya hewa.
Mwito huo umetolewa baada ya Marekani kuanza mchakato wa kujitoa rasmi kwenye makubaliano ya Paris, na kuifanya kuwa nchi pekee duniani kati ya pande 200 zilizosaini makubaliano hayo. Kwenye jarida la BioScience la Marekani wanasayansi wa Marekani wameonya kuwa kama hatua hazitachukuliwa binadamu watateseka kutokana na hewa zinazotolewa na viwanda.
Wametoa mwito wa kubadili matumizi ya nishati za visikuku kwa nishati endelevu zenye uchafuzi mdogo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |