Kamati ya kwanza ya Baraza kuu la Umoja wa Mataifa imepitisha maazimio matatu yaliyopendekezwa na Russia ya kuzuia ushindani wa kijeshi kwenye anga ya juu. Maazimio hayo ni pamoja na "hatua halisi za kuzuia ushindani wa kijeshi kwenye anga ya juu", "kutoweka silaha kwanza kwenye anga ya juu", na "uwazi na hatua za kujenga uaminifu". Marekani na Israel ni nchi pekee zilizopiga kura ya hapana dhidi ya maazimio hayo yote.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |