Waziri wa mambo ya nje wa Russia Bw. Sergei Lavrov amesema, hatua za kipindi cha nne zilizotangazwa na Iran za kusitisha utekelezaji wa makubaliano ya nyuklia JCPOA, ni kupunguza wajibu wake wa kutekeleza makubaliano hayo, bila kukiuka mkataba wa kutoeneza silaha za nyuklia. Amesema, kwa mujibu wa azimio la Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa wajibu wa Iran katika kutekeleza makubaliano hayo ni wa hiari, unaotegemea nchi nyingine kutekeleza wajibu wao au la.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |