Rais Xi Jinping wa China atafanya ziara ya kiserikali nchini Ugiriki na Brazil, na kuhudhuria mkutano wa kilele wa 11 wa BRICS utakaofanyika katika mji mkuu wa Brazil, Brasilia.
Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Bi. Hua Chunying amesema, rais Xi atafanya ziara hiyo kuanzia tarehe 10 hadi 15 mwezi huu.
BRICS ni kundi linaloibuka kiuchumi na linajumuisha nchi za Brazil, Russia, India, China, na Afrika Kusini.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |