Real Madrid wanaangalia uwezekano wa kutoa malipo makubwa kuwahi kushuhudiwa ya pauni milioni 340 kwa ajili ya mchezaji wa safu ya ushambulizi wa Paris St Germain mwenye umri wa miaka 20 Kylian Mbappe. Huo utakuwa usajili mkubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa katika historia ya soka kwa kuwa anayeshikilia rekodi ni Neymar ambaye alisajiliwa kwa dau la pauni milioni 200 wakati Ronaldo akienda Juventus kwa pauni milioni 105.