Waraka ulioandikwa na rais Xi Jinping wa China kuhusu nadhari za Umaksi utachapishwa kesho katika toleo la 22 la jarida la Qiushi la mwaka huu.
Waraka huo ni maandishi ya hotuba ya rais Xi aliyoitoa kwenye kikao cha tano cha Baraza la 19 la Mashauriano ya Kisiasa la Chama cha Kikomunisti.
Taarifa iliyoolewa na Shirika la Habari la China Xinhua imesema, hotuba hiyo ilihusu "Ilani ya Kikomunisti" na umuhimu wake mkubwa, ambapo rais Xi alitoa wito wa kuongeza juhudi kuendeleza uelewa mkubwa wa mchango wa Ilani ya Kikomunisti na athari yake kwa harakati za kijamaa duniani, na pia kushikilia kanuni na moyo wake.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |