Vikosi vya Uturuki na Russia vimefanya duru ya 9 ya doria za pamoja kaskazini mwa Syria kufuatia mpango uliofikiwa mwezi uliopita wa kuondoa wapiganaji wa Kikurdi. Tarehe 22 Oktoba, Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki na mwenzake wa Russia Vladimir Putin walifanya mkutano huko Sochi, Russia, wakikubaliana kuwaondoa wapiganaji wa kikundi wa YPG kwenda kilomita 30 kusini mwa mpaka wa Uturuki ndani ya saa 150, na kuzindua doria za pamoja za askari wa Uturuki na Russia katika sehemu iliyokubaliwa ikiwemo mji wa Qamishli ambayo iko kilomita 10 kutoka mpaka wa Uturuki.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |