Ethiopia na Djibouti zimejiandaa kuadhimisha miaka miwili tangu kuanza kazi kwa reli ya kwanza ya umeme barani Afrika iliyojengwa na kampuni mbili za China.
Shirika la Utangazaji la Ethiopia (FANA) limesema, waziri wa uchukuzi nchini humo Dagmawit Moges na Waziri wa Vifaa na Uchukuzi wa Djibouti Moussa Mohammed Ahmed wamejadiliana mafanikio ya reli hiyo katika miaka miwili iliyopita na pia mipango ya baadaye, ikiwemo kugharamia kwa pamoja mradi huo.
Reli hiyo ilijengwa na kampuni mbili za China na kuunganisha Ethiopia, nchi isiyo na bandari, na Djibouti, ambayo iko kando ya Bahari Nyekundu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |