Waziri mkuu wa China Bw. Li Keqiang hapa Beijing amefanya mazungumzo ya nne ya meza duara ya "1+6" na wakuu wa mashirika makuu ya fedha ya kimataifa ikiwemo Benki ya Dunia, Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Shirika la Biashara Dunia(WTO)na Shirika la Kazi la Umoja wa Mataifa, ILO.
Mkutano huo wenye kaulimbiu ya "Kuhimiza uwazi, utulivu na maendeleo ya sifa ya juu ya uchumi wa dunia" umefanya mawasiliano ya kina juu ya mustakabali wa uchumi wa dunia na hatua za kukabiliana na hali mbalimbali, kuhimiza usimamizi na mageuzi ya dunia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |