Mratibu wa misaada ya dharura wa Umoja wa Mataifa Bw. Mark Lowcock amekwenda Sudan ambako watu milioni 8.5 wanahitaji misaada kutokana na msukosuko wa kiuchumi na milipuko ya ugonjwa.
Msemaji wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Stephane Dujarric amesema, ziara ya Bw. Lowcock itaanza tarehe 22 hadi 24 mwezi huu, ambapo atakutana na maofisa wa Sudan na wafanyakazi wa haki za binadamu nchini humo.
Bw. Dujaaric pia amesema Bw. Lowcock atakwenda jimbo la Kassala kuangalia miundo mbinu ya afya na kuzungumza na watu walioathiriwa na matatizo yaliyopo, na watu wanaojitolea kukabiliana na hali hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |