Wauzaji wa bidhaa za chakula nchini Rwanda wamelalamikia kupanda kwa bei za bidhaa hizo.
Wafanyabishara katika mkoa wa Kusini kwenye masoko ya Gikondo, Nyabugogo na Huye, wanasema baadhi ya bei ya vyakula imepanda mara dufu.
Wadau wa kilimo wanasema kupanda kwa bei kumechangiwa na mvua inayonyesha kupita kiasi na kuharibu mimea.
Bidhaa zilizopanda bei ni kama vile maharage, mahindi viazi na mboga.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |