Kampuni ya Umeme nchini Afrika Kusini Eskom imezilaumu mvua zinazoendelea kunyesha kwa kusababisha umeme kukatika mfululizo kwa siku tano.
Kutokana na mvua hizo, baadhi ya vituo vya kuzalisha umeme vya kampuni hiyo vimefurika na kusababisha mashine kutofanya kazi vizuri, hivyo kuathiri upatikanaji wa umeme.
Tatizo hili limekuja wakati nchi hiyo tayari inakabiliwa na kushuka kwa uchumi wake, na litaathiri zaidi ukuaji wa uchumi wa nchi hiyo wakati ikielekea kwenye msimu wa sikukuu na wakati ambao watalii wengi wanapenda kutembelea nchi hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |