Wiki moja tu baada ya kutunukiwa Shahada ya Heshima katika masuala ya Sayansi kutoka Chuo Kikuu cha Laikipia, mshikilizi wa rekodi ya dunia ya mbio za Marathon Eliud Kipchoge anatazimiwa kutuzwa tena Shahada ya Heshima ya Sheria hii leo katika Chuo Kikuu cha Exeter nchini Uingereza. Chuo hicho kimetangaza kuwa, kitamkabithi mwanariadha huyo cheti hicho wakati wa sherehe yake ya kufuzu kwa mahafali. Baraza la seneti la chuo hicho limemtambua bingwa huyo kwa ufanisi wake kwenye nyanja ya michezo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |