Mkutano mkuu wa mwaka wa kazi za kiuchumi wa China umeamua kuwa mwakani China itaimarisha mageuzi ya mfumo wa kiuchumi.
China pia itaongeza kasi ya kuyafanyia mageuzi makampuni ya serikali na kuboresha matumizi ya mitaji ya kiserikali inayomilikiwa na taifa. Pia itaboresha mazingira ya biashara ya makampuni binafsi, na kutatua tatizo la ugumu wa kukusanya fedha.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |