Manchester City itavaana na mahasimu wake Manchester United katika mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Ligi. Wakati miamba hiyo ikitarajiwa kutoana jasho, Leicester City itakutana na Aston Villa katika mechi nyingine ya mashindano hayo. Katika mechi hizo, Man United itakuwa nyumbani Old Trafford kama ilivyo kwa Leicester City ambayo itakuwa King Power. Man City iliichapa timu ya daraja la kwanza Oxford United bao 3 – 1 huku Man United ikiilaza Colchester United ya daraja la pili bao 3 – 0.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |