Beki bora kabisa duniani kwa sasa, Virgil van Dijk amefunguka kuhusu kukosa tuzo ya mchezaji bora Ballon d'Or huku akisema namna alivyohuzunishwa kwa kuikosa wakati akishuhudia ikienda kwa nyota wa Barcelona, Lionel Messi. Van Dijk anayekipiga ndani ya klabu ya Liverpool alizidiwa kura saba (7) pekee mbele ya mchezaji bora kabisa duniani kwa sasa, Lionel Messi katika tuzo hizo. Mchezaji huyo mwenye jina kubwa kwa sasa barani Ulaya, aliuambia mtandao wa Mirror kuwa alijua mapema hatokwenda shinda tuzo hiyo ya Ballon d'Or hata kabla ya kufanya maamuzi ya kwenda kwenye sherehe hizo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |