Mshambuliaji wa Liverpool Sadio Mane amembwaga mwezake Mohamed Salah na staa wa Man City Riyad Mahrez kutawazwa mchezaji bora Bara Afrika wa mwaka 2019. Mane alitangazwa mshindi wa tuzo hilo maridadi wakati wa hafla ya utoaji tuzo iliyofanyika jana usiku mjini Hurghada, Misri. Hii ilikuwa mara ya nne kwa mzawa huyo wa Senegal kujaribu kushinda tuzo hiyo, baada ya kushindwa kutwaa ushindi mara tatu. Mane alifurahia mwaka mzuri wa ufanisi katika klabu yake na pia timu yake ya nyumbani, kwa kusaidia Liverpool kushinda kombe la UEFA.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |