Mabingwa wa mwaka 1988 wa Ligi Kuu Tanzania, Coastal Union imepanda hadi nafasi ya pili baada ya kuichapa Kagera Sugar huku Lipuli ikilazimisha sare ya bao 1 – 1 KMC. Coastal wakiwa kwenye uwanja wa nyumbani wa Mkwakwani, Tanga, walifanikiwa kupata ushindi wa bao moja katika dakika ya 77 na kuwafanya kufikisha point 29 na kuishusha Azam yenye point 26. Lipuli nayo imepoteza nafasi ya kupanda hadi nafasi ya tatu baaa ya kukubali kulazimishwa sare ya bao 1 – 1 na timu ya KMC katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru. Simba imeendelea kuongoza Ligi hiyo ikiwa na pointi 35.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |