Kipa wa timu ya Taifa ya Wanawake ya Kenya Harambee Starlets, Annedy Kundu amesaini mkataba wa miaka mitatu na klabu ya Lakatamia inayocheza ligi ya wanawake ya Cypriot nchini Cyprus. Annedy pamoja na mchezaji mwenzake wa Harambee Starlets Ruth Ingozi wanaondoka nchini Kenya hii leo kuungana na wenzao wa klabu ya Lakatamia ya Cyprus. Annedy alionekana wakati wa mashindano ya CECAFA ya wanawake mwaka jana yaliyofanyika nchini Tanzania, na aliokoa mikwaju kadhaa iliyoifanya timu yake kushinda mashindano hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |