Kwa mujibu wa ripoti ya utendaji kazi wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa mwaka 2019 iliyotolewa jana, Baraza hilo lilifanya mikutano 258, kupitisha maazimio 52 na kutoa taarifa 15 za mwenyekiti. Ripoti inasema Baraza hilo lenye majukumu ya msingi katika kulinda amani na usalama wa kimataifa, lilijadili ajenda 49 na kutuma ujumbe katika nchi mbalimbali zikiwemo Ethiopia na Sudan Kusini.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |