Jeshi la Algeria limefanya luteka katika mpaka na Libya chini ya usimamizi wa mkuu wa mpito wa jeshi Said Chengriha. Wizara ya Ulinzi ya Algeria imesema Chengriha leo atafanya ziara katika eneo la nne la kijeshi la Quargla, si mbali na mpaka na Libya, akifuatilia utekelezaji wa mpango wa mapambano wa vitengo vya jeshi katika maeneo yote ya kijeshi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |