Hali ya kawaida imerejea katika mji mkuu wa Sudan, Khartoum, Jumatano, baada ya siku moja ya uasi uliofanywa na kundi lililo chini ya Idara Kuu ya Upelelezi. Mnadhimu mkuu wa jeshi la Sudan Mohamed Osman Al-Hussein amesema, wanajeshi wawili wameuawa na wengine wanne kujeruhiwa, wakiwemo maofisa wawili, wakati wa operesheni ya kudhibiti tena jengo la Idara Kuu ya Upelelezi (GIS).
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |